06/10/2024
*MFUMO WA _P*S_ NI STENDI KIGANJANI MWAKO*
Ndugu Abiria,
Umewahi kusikia kuhusu mfumo wa P*S? Basi k**a hujawahi kusikia, fahamu kuwa LATRA sasa wamekuletea stendi kiganjani mwako. Kwa kutumia mfumo wa P*S, unaopatikana katika kiungo (link) cha https://pis.latra.go.tz/, sasa hivi unaweza kujua na kufanya yafuatayo:
1. *Kujua muda ambao basi litawasili katika kituo unachotaka kuanzia safari au kulisubiria*;
2. *Kujua muda unaotarajia kufika kule uendako*;
3. *Kujua mwendokasi wa gari unalosafiri nalo au jingine lolote lililopo barabarani*
4. *Kujua jina la mmiliki wa gari husika litakalowasili kwenye kituo ulichopo*
5. *Kujua kituo cha mwisho gari lililokuwepo au lilipo kwa muda huo kabla ya kufika ulipo au kule linakoelekea*
Taarifa hizo pia zitakuwa zinapatikana kupitia skrini (screens) zilizopo kwenye vituo vyote vikuu vya mabasi. Baada ya kupata taarifa unayohitaji sasa ni rahisi kwako kuingia kwenye mfumo wa basi husika na kukata tiketi, ikiwa shida yako ilikuwa kusafiri au kuendelea kumsubiria mgeni wako, au kujiridhisha tu.
Ni rahisi sana kutumia. Chukua simu yako ya kiganjani ingia kwenye Google au Mozilla firefox, andika https://pis.latra.go.tz/ au P*S LATRA kisha, tafuta (search), mfumo utafunguka na kukuleta ukurasa wa kwanza utakaokuwa na sehemu mbili: Vituo vya Mabasi (Bus Stations) na Mwendokasi wa Basi (Bus Speed). K**a unataka kujua ratiba ya kuwasili kwa basi husika basi bonyeza Vituo vya Mabasi kisha huko ndani utachagua kituo husika. K**a unataka kujua mwendo wa basi unalosafiria basi bonyeza mwendokasi wa basi. Hapo utaingiza namba ya basi husika kisha itakuletea taarifa nzima ya mwendokasi wa basi hilo kwa siku ulizochagua.
Kutokana na ukweli kuwa sasa unaweza kujua basi fulani liko wapi au litawasili muda gani, na kutokana na ukweli kuwa unaweza kukata tiketi mtandaoni kwa kutumia link ya mtandao wa basi husika, kazi ya stendi za mabasi imeanza kupungua siku hadi siku. Kazi pekee iliyobaki ni kuwa kituo cha kusubiria gari tu au kushukia.