Africa moto

Africa moto Ni page ya kiburudani inayo kupa habari mbali mbali za wananamuziki wa bend za kitanzania na kiafrica pia

15/07/2017

HII tafsiri yake ni kwamba MSONDO ndiyo baba ya muziki na ndiyo nyumbani kwa wanamuziki wote mastaa wa dansi waliopata kupitia hapo?
1. Nico Zengekala alifariki akiwa Msondo!
2. Suleiman Mbwebwe alingia Msondo anazunguka Vijana Jazz na kweingineko, akarejea nyumbani na kufariki akiwa Msondo!
3. Athumani Momba alijiunga Msondo akitokea Bima, aliondoka na kwenda Vijana Jazz, akarejea tena nyumbani na akafariki akiwa Msondo!
4.Joseph Maina alifariki Msondo!
5. Tx Moshi William aalifariki akiwa Msondo!
6. Muhidini Gurumo aliasisi NUTA, lakini akaondoka mwaka 1978 kwenda Sikinde, 1985, Ndekule, akarejea nyumbani kwake Msondo 1990. Naye alifariki akiwa Msondo.
7. Dede alikuwa Msondo, akatoka kwenda Sikinde, Bima, akarejea Msondo akatoka, akaenda OSS, Bima, Sikinde, lakini nyumbani ni nyumbani akarejea Msondo. Akafariki akiwa Msondo.
Unaonyesha kuwa wanamuziki huwa wanatoka Msondo kwenda kutafuta, lakini baadaye wanarejea nyumbani kwao. Na ndiko wanakopumzikia hadi Mungu anawachukua.

30/06/2017

Remmy Ongala Alikuwa kipenzi cha watu aliyewaacha wapenzi wake na wananchi kwa ujumla katika dimbwi la majonzi yasiyosahaulika kufuatia tungo za nyimbo zake zenye maudhui maridhawa, ambazo hadi leo zinarindima katika vituo vingi vya redio hapa nchini hata nje ya mipaka yetu
Dk. Remmy alikuwa wa kwanza kupata ujasiri wa kukemea ngono zembe, akatunga wimbo ‘Mambo kwa soksi’ Lakini jamii ikambeza kwamba wimbo huo haukuwa na maadili mema. Baadaye viongozi wa serikali,vyama na dini na wengine kwa ujumla walielewa nini alichokuwa akisema Dk. Remmy, wakaanza kuhubiri majukwaani tahadhari hiyo.
Alizaliwa akiwa na meno mawili ya mbele kinywani mwake na akaonekana kana kwamba ni mtoto wa ajabu. Aidha hakuwahi kunyolewa nywele zake kwa miaka yote hadi alipokuja kuokoka akiwa hapa nchini Tanzania
Dk. Remmy alijipatia umaarufu katika jiji la Dar es Salaam hususan maeneo ya Sinza. Alikuwa na gari yake ndogo ‘soloon’ lililokuwa la aina yake popote lipitapo watu walilishangaa. Lilikiwa na maandishi nyuma ya gari hilo yakisema ‘ Baba yako analo’?
Historia ya maisha ya Dk.Remmy Ongala yaelezwa kwamba mara Dk. Remmy Ongala alipozaliwa, wazazi wake walimuita Ramadhani Mtoro Ongala. Alizaliwa mwaka 1947 katika mkoa wa Kivu huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Familia yake iliishi katika eneo lililoitwa Kindu eneo ambalo halikuwa mbali sana kutoka mpakani na Tanzania.
Baba yake alikuwa ni mwanamuziki mashuhuri pia alikuwa mpiga ngoma kwa kutumia mkono na pia mbira. Baada ya kuzaliwa kwake haikuchukua muda mrefu familia yake ilihamia katika mji wa Kisangani huko DRC.

Ipo habari kwamba kabla ya kuzaliwa kwake, mama yake alipata ujauzito mara mbili lakini kwa bahati mbaya kila alipojifungua, mtoto alifariki. Alipopata ujauzito mara ya tatu alienda kwa mganga wa kienyeji kumuomba ushauri afanye nini ili mtoto atakayezaliwa asiiage dunia pia.

Bila kusita mganga wa kienyeji akampa ushauri wake. Akamwambia kwanza safari hii asiende kujifungulia hospitali bali akajifungulie maporini. Pia alipewa ushauri kwamba mtoto akishazaliwa asije akamkata nywele zake. Yote hayo yalitendeka na ndio kisa cha Dk. Remmy Ongala kutokata nywele hadi alipozidiwa na maradhi yaliyompelekea kuokoka ndipo aliponyoa nywele zake akiwa hapa nchini Tanzania.

Mwenyewe aliwahi kusema kwamba mwanzoni alikuwa anajisikia aibu sana kwa kuwa na nywele ndefu namna ile. Lakini baadaye jina na taswira ya mfalme wa reggae ulimwenguni, hayati Bob Marley ilipopata umaarufu nchini Congo, ndipo alipoipenda staili ile ya nywele kwani hata watu wengine pia walianza kuikubali na kuionea ufahari.

Pia inasemekana Remmy alizaliwa akiwa tayari na meno mawili ya mbele kitu ambacho kilichukuliwa k**a ishara ya baadaye kuja kuwa mganga wa kienyeji. Ingawa utabiri huo haukutimia, inasemekana huo ndio mwanzo wa yeye kujulikana hapo baadaye k**a Doctor Remmy Ongalla.

Baba yake ndiye aliyeanza kumfunza mambo ya muziki tangia akiwa mdogo kabisa. Jambo lililomfanya aamini kabisa kwamba k**a jinsi ambavyo watu wengine wamezaliwa kuwa madaktari, wanasheria, waalimu, wakulima nk, yeye alizaliwa ili awe mwanamuziki.

Kwa bahati mbaya baba yake huyo mwaka 1953 alifariki dunia na kumuacha Remmy akiwa na miaka sita, akiwa tayari ameshaanza shule. Lakini kutokana na ukosefu wa fedha na kwa sababu mama yake hakuweza kuendelea kumlipia karo za shule, Remmy ilibidi aache shule.

Ilipofika miaka ya 1960, Remmy tayari alikuwa ameshajifunza mwenyewe kupiga gitaa.
Mwaka mmoja baada ya kifo cha Baba yake mzazi, mwaka uliofuatia wa 1964 ulikuwa si mzuri kwa Remmy kwani mama yake mzazi naye alifariki dunia jambo ambalo lilimuacha Remmy na mzigo wa kuwalea wadogo zake kwani yeye sasa ndio alikuwa mkuu wa familia licha ya umri wake mdogo.

Bila elimu na ujuzi mwingine wowote, alilazimika kuanza rasmi kujitafutia riziki kupitia muziki. Ujuzi wake wa kupiga gitaa uliongezeka kwa kasi ya ajabu kitu ambacho kilimuwezesha kutumbuiza kwa kupiga ngoma na gitaa katika hoteli nyingi na sehemu mbalimbali nchini ya Congo akiwa na bendi yake iliyokuwa imesheheni vijana wenzake iliyoitwa ‘Bantu Success’.

Kwa miongo kadhaa iliyofuatia Dk. Remmy Ongala alizunguka katika sehemu mbalimbali za Congo akiambatana na bendi kadhaa maarufu za wakati huo nchini Congo zikiwemo Success Muachana na ile ya Grand Mickey Jazz nchini Uganda.

Japokuwa kwa ujumla Dk. Remmy alijifunza mwenyewe kupiga gitaa, lakini aliwahi kukiri kwamba muziki wa kutoka nchini Cuba ambao wakati huo ulikuwa unaanza kujipatia umaarufu barani Afrika, ulimsaidia katika kupata staili ya pekee katika upigaji gitaa.

Kwa upande wa uimbaji anasema uimbaji wa Joseph Kabasele ‘Grand Kale’ na ule wa Franco Lwambo Makiadi ulimsaidia kupata staili yake ya uimbaji k**a tulivyoizoea kusikia enzi za uhai wake.

Mwaka 1978 Remmy aliingia jijini Dar es Salaam baada ya kuitwa na mjomba wake mzee Kitenzogu Makassy ili aje ajiunge na bendi maarufu ya wakati huo ya Orchestra Makassy, iliyokuwa chini ya uongozi wa mjomba wake huyo.

Huo ukawa ndiyo mwanzo wa maisha ya Dk. Remmy nchini Tanzania. Akiwa na bendi ya Orchestra Makassy, alitunga wimbo wake wa kwanza uliojulikana k**a ‘Siku ya Kufa’, wimbo ambao aliuandika kumkumbuka rafiki yake aliyefariki. Wimbo huo ulianza kumpatia umaarufu mkubwa na kujulikana kwa haraka hapa nchini.

Mzee Makassy aliamua kuihamishia bendi yake keipeleka nchini Kenya, kitendo hicho cha mjomba wake kilichomfanya Dk. Remmy kujiunga na bendi ya Matimila baada ya kudumu kwa katika bendi ya Orchestra Makassy kwa takriban miaka mitatu hivi.

Jina la bendi hiyo ya Matimila lilitokana na jina la kijiji kimoja kilichoko kusini mwa Tanzania. Kujiunga kwa Remmy katika bendi ya Matimila, alijiongezea umaarufu katika anga za muziki nchini Tanzania wakati huo. Chini ya uongozi wake Dk. Remmy aliisuka upya bendi hiyo na kuibadilisha jina ikaitwa Orchestra Super Matimila.

Miaka iliyofuatia Watanzania tulishuhudia umaarufu wa Remmy ukiongezeka hususan kutokana na mashairi ya nyimbo zake ambayo yaliegemea katika kuzungumzia mambo halisi ya kijamii k**a vile umasikini, afya, siasa , majanga ya Ukimwi nk.

Mafanikio ya Remmy na kundi lake zima la Orchestra Super Matimila hayakuishia nchini Tanzania kwani katika miaka ya mwishoni ya 1980 walianza kujipatia umaarufu nje ya mipaka ya Tanzania na Afrika.

Dk.Remmy Ongala aliwahi kusema kwamba kupata mialiko ya nje lilikuja k**a mchezo tu. Kasseti yenye nyimbo zao rafiki yake mmoja mzungu aliyekuwa akiondoka nchini Tanzania kurejea kwao Uingereza.

Rafiki yake huyo alipofika huko aliwapatia jamaa wa WOMAD (World of Music, Arts and Dance) shirika linalopandisha chati wanamuziki na wasanii mbalimbali kutoka katika nchi za dunia ya tatu. WOMAD walivutiwa na nyimbo zao, hivyo kuwapa mwaliko kushiriki katika maonyesho yao barani Ulaya ya mwaka 1988.

Baada ya kurudi kutoka Ulaya bendi ya Super Matimila ilitoa album yenye jina la ‘Nalilia Mwana’ ikiwa na mkusanyiko wa nyimbo zao zilikuwemo nyimbo zilizopendwa sana k**a vile ‘Ndumila Kuwili’ na ‘Mnyonge Hana Haki’

Mwaka 1989 Remmy na Matimila walirudi tena Ulaya kufuatia mwaliko mwingine wa WOMAD. Ni wakati huo huo ambapo walipata nafasi ya kurekodi kwenye studio ya kisasa zaidi ya Stud Real World Studios,
ambayo ilikuwa inamilikiwa na mwanamuziki maarufu aitwaye Peter Gabriel.

Dk. Remmy aliwahi kufafanua kuwa wimbo maarufu ya ‘Kipenda roho’ aliuimba mahsusi kwa ajili ya mkewe ambaye ni ‘mzungu’ muingereza ambaye wakati huo tayari walikuwa wameshazaa naye watoto watatu.

Mwaka 1990, Remmy na bendi yake ya Super Matimila walirejea tena katika studio za Real World ambako walirekodi album nyingine yenye nembo ya ‘Mambo’ ambayo ilikuwa na nyimbo k**a hiyo ya ‘Mambo’ ambayo aliimba kwa lugha ya kiingereza na kuweza kukidhi kiu ya wapenzi wake wasiojua Kiswahili. Zingine ni pamoja na ‘No money, no life’ na ‘One World’.

Umaarufu wake ulizidi kung’ara mwaka 1990 alipotoa wimbo wa ‘Mambo kwa soksi’ ingawa baadhi ya watu waliupinga kwa kusema kwamba haukuwa na maadili mema kwa jamii, ingawa kimsingi alikuwa anawaasa watu hususani vijana kutumia kondomu ili kuepukana na maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.

Akiwa Super Matimila Dk. Remmy alitoka na nyimbo ningi zikiwemo za ‘Bibi wa mwenziyo’, ‘Kipenda roho’, ‘Asili ya muziki’ na ‘Ngalula’. Zingine ni pamoja na ‘Mwanza’, ‘Mama nalia’, ‘Harusi’, ‘Hamisa’, ‘Mnyonge hana haki’, ‘Ndumila kuwili’ na ‘Mataka yote’ ambazo zilimuongezea sifa kubwa Dk. Remmy kufuatia maudhui yaliyokuwa yakikidhi jamii.

Baadaye Dk. Remmy Ongala akaanza kusumbuliwa na maradhi ya kisukari iliyompelekea kuamua kuachana na muziki wa dansi kwa madai ya kwamba umejaa mambo mengi ya kishetani.
Remmy akaokoka, akatubudu dhambi zake na akaanza kupiga muziki akimuimbia bwana.
Kabla ya kifo chake Dk. Remmy alitoa albamu yake ya Injili aliyooiita ‘Kwa Yesu kuna furaha’. Remmy alikuwa katika hatua za mwisho za kukamilisha albamu yake ya pili, lakini mungu akampenda sana usiku wa kuamkia Jumatatu ya Desemba 13, 2010 nyumbani kwake Sinza. Eneo hilo alilokuwa akiishi lilipewa jina la ‘Sinza kwa Remmy’ kufuatia umaarufu wake alipokuwa hai.

Mungu aiweke roho yake pahala pema peponi, Amina.

29/06/2017

HISTORIA YA WANYATURU.

WANYATURU ambao awali walijulikana kwa jina la Warimi ni watu wanaoishi karibu wilaya zote za mkoa wa Singida yenye wilaya saba.

Kwa Mujibu wa Patrick Mdachi katika kitabu cha Wanyaturu wa Singida, Mila na Desturi zao, Wanyaturu ni moja ya makabila yanayojumlishwa katika kundi la Nilo-Hamites, lenye asili ya Wabantu walioishi Abysinia ambayo sasa inajulikana k**a nchi ya Ethiopia.

Watu hao waliihama Abysinia (Ethiopia) kutokana na njaa kubwa kiasi ambacho hawakuweza kustahimili kukaa tena hapo. Njaa ndiyo iliwalazimisha watu hao kufikia kula nzige, katika harakati za kutafuta nzige hao ndio ukawa mwanzo wa safari yao ya kuhama.

Mdachi anasema katika kitabu chake hicho kilichochapishwa na Benedictine Publicationss Nandanda - Peramiho mwaka 1991, kuwa Wanyaturu waliingia Tanzania kupitia sehemu ya kaskazini kutokea Kenya na Uganda na kufanya maskani yao eneo la Uzinza, Mwanza, baadaye walihamia eneo la Pasiansi na mwaka 1700 walikutwa na Wasukuma ambao waliwafukuza na kuwafanya wakimbilie Ntunzu.

Baadhi ya watu hao (yaani Mwilwana na Masanja) wakiwa na wake zao na watu wengine wa kuwasaidia kazi hawakuweza kukaa Ntunzu, waliendelea na safari pamoja na ng’ombe wao mpaka mkoani Singida, eneo la mashariki lijulikanalo k**a Sepuka.

Mdachi anasimulia kwamba Wanyaturu hao walikaa hapo kidogo na ndio eneo hilo ambalo watu hao waligawanyika tena, lengo likiwa ni kupeana nafasi ya kilimo, ufugaji na kuweka makazi ya kudumu. Mwilwana akielekea kaskazinimashariki eneo la Ilongero ambapo alistawisha makao yake hapo na hapo ukawa mwanzo wa Mwilwana huku Masanja akienda upande wa mashariki eneo la Kisaki na kujenga juu ya jiwe liitwalo Wahi, anasimulia Mdachi.

Kwa mujibu wa masimulizi hayo, Masanja alijaaliwa kuwa na watoto wanne ambao aliwapa majina yao kulingana na kazi walizofanya au tabia. Watoto hao ni Sengasenga aliyepewa jina hilo kutokana na kuwa baba yao alipoanza akiwa maskani alifyeka mapori. Kufyeka pori kwa Kinyaturu ni ‘Usenga’.

Mtoto mwingine aliyefuatia aliitwa Mpuma ambaye alipewa jina hilo kutokana na eneo hilo kuwa na tumbili wengi. Mpuma kwa Kinyaturu ni tumbili. Mtoto wa tatu alipewa jina la Hati kutokana na jiwe ambalo baba yao alitumia kujenga nyumba na wa mwisho alijulikana kwa jina la Mkahiu kutokana na furaha ya wazazi wao.

Watoto hawa walitawanyika ikiwa ni suluhu ya ugomvi wao na kila mmoja alianzisha ukoo wake ambazo zilikuja kujulikana k**a Senga, Anyahati, Puma na Ukahiu. Utafiti unaonesha kuwa jina la kabila la Wanyaturu ni la hivi karibuni, awali kabila hili lilijulikana k**a Warimi. Jina hilo walipewa na watani wao Wanyamwezi ambao walikuwa wakiwinda pamoja.

Siku moja wakiwa katika kuwinda walimpiga mshale wa sumu mnyama wa porini, mnyama huyo akakimbia na Wanyaturu wakiwa wanamkimbiza walikuwa wakisema ‘Mughuu turu, turu’ wakimaanisha mguu huu hapa.

Wanyamwezi wakaanza kuwaita Banyaturu jina likaendelea kukolea mpaka leo wanaitwa kwa jina hilo na lile lao la asili, yaani Warimi, likapotea. Wanyaturu ni watu wanaopakana na makabila ya Wanyiramba na Winyisanzu (magharibi), Wamang’ati ambao pia huitwa Wabarbaig (kaskazini-mashariki), Wasandawe (mashariki), Wagogo (kusini) na Wanyamwezi na Wasukuma upande wa Kusinimagharibi.

Muundo wa utawala wa Wanyaturu Mfumo wa utawala wa kisiasa wa kabla na baada ya kuingia wakoloni unahusu imani na utaratibu wa dini za kiasili. Tofauti na makabila mengi hapa nchini, Wanyaturu hawakuwa na utawala wa kichifu. Katika kabila hili kila ukoo ulikuwa na wazee (ambao kwa siku hizi tungewaita halmashauri) ambao kazi yao kubwa ilikuwa ni kushauri pamoja na kupatanisha mashauri mbalimbali.

Koo zinapokuwa nyingi zilipata kiongozi mmoja ambaye alichaguliwa kutokana na kazi yake, pamoja na ujasiri wake wa kivita. Uongozi wa namna hiyo haukuwa wa kurithi, bali ulipatikana k**a Wanyaturu wanaovyoamini hutokana na bahati au neema ya jua.

Jinsi kiongozi anavyopatikana husemakana kuwa na nyota ya pekee sana hasa kutokana na kuwa na waganga au waaguzi ambao humsaidia katika kazi zake. Waaguzi hao ambao huchaguliwa kutoka kwenye ndoto na uteuzi wake hujulishwa na miungu au mungu mwenyewe na kazi yao kubwa ilikuwa ni kutabiri mambo ya baadaye katika jamii.

Hivyo kumfanya kiongozi kutekeleza mambo yake kwa mwongozo wa ndoto za waganga hao. Waaguzi hao ndio waliokuwa viongozi wa kiroho. Kila kiongozi wa kivita alikuwa na kiongozi wake wa kiroho ambaye pia alikuwa akimpa dawa za kinga. Mganga au muuguzi mkuu alikuwa akiitwa Saigiro ambaye inasemekana alikuwa akitoka kabila la Tatong.

Ujio wa wakoloni Stanley alionekana katika eneo la Wanyaturu mwaka 1874 baada ya kuweka bomba na chuma juu ya jiwe la Damankia, eneo la Dung’unyi, katika tarafa ya Ikungi. Stanley alitanguliwa na Waarabu ambao inasemakana walikuwa wa kwanza kukanyaga ardhi ya Wanyaturu. Hawa walikwenda kutafuta mtama.

Watu hao wote waliwaona Wanyaturu kuwa ni watu wanaopenda vita. Mwaka 1900 ndio mwaka ambao Wajerumani walianza kuingia taratibu na mbinu waliyoitumia kuingia ilikuwa ni kwa kuwavutia viongozi wa vita ambao walikwenda k**a wajumbe wa biashara ya ng’ombe na mtama kwa nguo na shanga.

Hata hivyo, ujio wa wakoloni, ulitabiriwa na mganga Sakilo ambaye aliishi katika mlima Hanah na ambaye alikuwa aidha anatoka katika kabila la Tatog au Kimbugwe ambao walitabiri ujio wa wekundu wasio na vidole miguuni, kwani walivaa viatu. Jina lingine walilopewa wazungu na Wanyaturu ni ‘Anyeke’, yaani watu walio na miguu k**a tunda bivu kutokana na kuvaa viatu.

Baadhi ya Wanyaturu hawaukufuatilia utabiri huo kutokana na kupendelea sana utabiri wa Mahindi wa Isuna ambaye alitabiri kuwa Maksai mwekundu alionekana katika maamkio yake na kukatokea vifo vingi, njaa, vitisho na fujo za kila namna. Kwa Wanyaturu rangi nyekundu ni hatari na ng’ombe mwekundu huwa hatumiki kwenye sadaka ya aina yoyote.

Karibu Singida.

_________👇____________

HISTORIA YA WANYATURU II.

Wanyaturu (au Waturu ; wao hupendelea kuitwa Arimi, yaani watu wa Rimi ni kabila la watu wa
Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Singida .
Lugha yao ni Kinyaturu, ambacho ni jamii ya Kibantu, lakini kina fonimu nyingi za Kikushi .
Historia
Asili ya kabila hilo inasemekana ni nchi ya Ethiopia ambako kunasadikiwa kuwa na watu wanaotumia lugha ambayo kwa asilimia kubwa inafanana na Kinyaturu. Hudhaniwa pia kuwa Wanyaturu na Wakushi wa Ethiopia asili yao ni moja.
Walipoingia eneo la Tanganyika walichangamana na Wanyatunzu pamoja na Wasukuma , ndiyo maana
mila na tamaduni zao zinashabihiana kwa kiasi kikubwa, hivi kwamba ni vigumu kumpambanua Mnyaturu baina ya Wanyatunzu.
Wana utani na Wanyiramba na
Wairaqw .
Idadi na mgawanyiko
Mwaka 1993 walikuwa 556,000 .
Ndani ya kabila hilo, kuna makundi matatu:
Vahi (Wahi) , ambao ni zaidi ya nusu ya Wanyaturu wote, na kuwa wenyeji wa mji wa Singida : hao wanaishi kuanzia Singida mjini hadi karibu na
wilaya ya Manyoni.
Airwana (Wilwana) wanaishi
kaskazini kwa ziwa Singida;
na lile dogo zaidi la Anyiŋanyi (Wanyinganyi) wanaoishi maeneo ya
Mnying'anyi .
Unyambwa pia ni sehemu iliyoko Singida na inasemekana ni ukoo mkubwa sana wenye mababu wakubwa wawili: mzee Ghambona na Hante. Ukoo huu hauvumi sana kutokana na watoto wa wazee hao kuhama Unyambwa na kwenda Iguguno, ambako lakini hawakukaa sana, wakahama tena na kuelekea hasa mikoa jirani k**a Shinyanga , Tabora na Mwanza . Ni ukoo wenye watoto wengi wa k**e kuliko wa kiume, na dini yao kubwa ni Uislamu .
Tanbihi
1. ↑ Pengine jina "Wanyaturu" linapoteza historia yao kwani liliundwa na Wazungu
2. ↑ Unaweza kubadilisha hapa kuhusu Airwana kuwa si wengi karibu nusu ya Wanyaturu wote kwa ukianzia pale mjini Singida ukielekea Kusini hadi sehemu za Issuna hadi Itigi na Manyoni hadi Kintinku hawa ni Vahi tu, bado sijasema sehemu za Ihanja hadi Muhintiri na sehemu za Mang'onyi na Misughaa ni vahi au wahi kwa hiyo robo tatu ya wanyaturu ni wahi yaani vahi waweza kufanya utafiti na utagundua ukweli huo. wairwana wana maeneo kuelekea Kaskazini ambayo ni sehemu ndogo sana kieneo na inapakana na Wanyiramba ukifika sehemu za Iguguno.
Tukiangalia asili ya kabila la Wanyaturu, utawala wao na ujio wa wakoloni kwa mujibu wa Patrick Mdachi katika kitabu chake cha Wanyaturu wa Singida, Mila na Desturi zao.
Kwa kifupi anasema kwamba Wanyaturu ni moja ya makabila yanayojumlishwa katika kundi la Nilo-Hamites, lenye asili ya Wabantu walioishi Abysinia ambayo sasa inajulikana k**a nchi ya Ethiopia. Leo tunaendelea na simulizi la kabila hilo kwa mujibu wa Mdachi katika kitabu hicho kilichochapishwa na Benedictine Publications Nandanda - Peramiho mwaka 1991.
Mdachi anaendelea kusimulia kwamba Wakoloni wa Kijerumani hawakuweza kuingia kirahisi katika ardhi ya Wanyaturu. Ujio wao kuliibua mvutano ambao ulitokea na kuenea sehemu za Iramba na Isanzu kutokana na jamii kutokubaliana na mfumo mpya wa siasa, jambo lililowafanya kugoma, mgomo uliotokea mwaka 1902.
Uchumi wa sehemu ya kusini mwa Singida ulitegemea ng’ombe pamoja na mtama. Wajerumani walijitahidi kubadilisha hali ya uchumi na kuleta hali mpya ya uchumi baada tu ya kuanzishwa msh*tuko katika maisha ya jamii. Hali hii ndiyo iliyofanya kuwapo kwa mgomo mkali kusini kuliko sehemu ya kaskazini.
Wanyaturu waliwachukia Wajerumani kwa sababu ya unyang’anyi wao na kuwaweka nguvuni baadhi ya viongozi wa kivita.Lingine lililowaudhi ni kuanzishwa kwa ukusanyaji wa kodi na kuanzisha matumizi ya sarafu ya mviringo iliyopigwa chapa ya Kilimatinde mwaka 1907. Kuna wengine walipinga hatua ya kuwapa nguo na kubadilishana kwa ng’ombe.
Katika kuonesha kuwa nguo hizo hazina thamani kwao, Wanyaturu wakazilinganisha na kuku kwamba ni sawa na mtu kumpa ng’ombe yeye akakupa kuku, Mdachi anasimulia. Katika mapambano hayo, Wanyaturu walionekana ni jasiri kutokana na jeuri iliyotokana na Mungu wa mvua ‘Tita’ na kuongozwa na utabiri.
Mbinu za Wanyaturu katika vita hii zilikuwa ni zile za maficho (porini) huku wakitumia mishale. Mathalani, majumbe walijikuta wamezingirwa kwenye duara na watu wenye mikuki yenye kutisha, matokeo ilikuwa ni kutolipwa kwa kodi na ilibidi wakusanyaji kodi watoe wenyewe kodi hizo ambapo walizilipiza kwa wanyonge zaidi.
Mfano mzuri wa mgomo wa Wanyaturu katika eneo la Wilwana, ni mwanamke aliyejulikana kwa jila na Leti wa Ughandi kuongoza mgomo wa Wanyaturu sehemu ya kaskazini. Alipinga utawala wa aina yoyote ule kutoka nje, hivyo kwa kutumia nguvu na msimamo wake alifuatwa na jeshi la Wakoloni, lakini kwa akili zake aliweza kutumia nyuki kulifukuza jeshi hilo.
Alichokuwa akifanya ni kwa kutumia nguvu zake aliweza kuwakusanya nyuki pamoja na hawa wakoloni walipotokea aliwafungulia nyuki ambao walishambulia na kulazimika kukimbia. Hata hivyo, kwa kutumia mbinu za kuzingira na kuteka nyara baadaye alishindwa kutokana na Wajerumani kutumia silaha za kisasa zaidi, yaani bunduki dhidi ya silaha zake za nyuki.
Maisha Kwa Wanyaturu mwanamke ana majukumu mengi katika jamii ikiwa ni pamoja na kulima, kuvuna, kupiga mtama, kuchanja kuni, kazi za jikoni. Kutokana na miiko, kazi kwa mwanamke mjamzito hupungua kwani anatengewa muda mwingi wa kupumzika hivyo kubakia na kazi ya jikoni na zingine ndogondogo.
Miiko kwa upande wa vyakula, mjamzito alikuwa haruhusiwi kula mayai (kwa dhana kuwa atazaa mtoto asiye na nywele) na pia hakuruhusiwa kunywa pombe kali (pombe ya asili), lakini vyakula vingine aliweza kula bila tatizo lolote. Baada ya kujifungua mama hupewa wasaidizi wa kazi na wengine wa kumkanda tumbo.
Muda huo mume hutayarisha mbuzi beberu ambalo huchinjwa na humpatia mkewe mchuzi (supu) k**a pole. Kwa upande wa wanawake wasiozaa yaani tasa, kwa Wanyaturu wanawake k**a hao huaminika kwamba kizazi chao kimechafuka. Ili kumsafisha, hupatiwa dawa ya kusafisha kizazi kutoka kwa mganga.
Mara nyingi walifanikiwa kuzaa na kikubwa iliaminika kwamba kutozaa ni mchezo wa kichawi. Ingawa maendeleo ya sayansi yanaonesha kuwa uzazi unaweza usifanyike kutokana na baba kuwa na matatizo, lakini kwa Wanyaturu mama ndiye alikuwa akinyooshewa kidole kunapotokea familia kukosa mtoto.
Wanyaturu wanathamini mwanamke anapozaa watoto wengi wakiamini, kuwa familia hiyo ina baraka nyingi za Mwenyezi Mungu ambazo huonekana kwa watoto wengi, na kwamba mtu huyo hupendwa na Mungu. Thamani nyingine ya watoto inatokana na kuamini kuwa ukoo huenea kwa haraka na kudumu kwa muda mrefu au kuendelea kwa kuwa na watoto wengi.
Kadhalika, kwa Wanyaturu kuwa na watoto wengi wa kiume kulionesha kupata ulinzi bora na wa kudumu katika familia. Pia mtoto wa kiume kwa Wanyaturu alichukuliwa kuwa ndiye atakayewatunza wazazi kuliko mtoto wa k**e, mlinzi wa familia yote na ndiye atakayeimarisha ukoo.
Kwa upande wa mama aliyezaa mapacha, hali ilikuwa tofauti, kwani anapojifungua mapacha hupigwa vigelegele (vinavyotokana na mlio baada ya kugongwa majembe) na huimbwa nyimbo fulani. Pia mzazi wa mapacha alifanyiwa karamu rasmi ambayo hujulikana k**a ‘Imma’.
Karamu hii hufanywa na wazazi au wajomba wa mama aliyejifungua wanapoenda kumpa pole kwa kumpelekea mbuzi na pombe ya asali.
Sherehe hiyo huishia kwa mume kutoa ng’ombe na kuwapa waliofanya sherehe hiyo. Hii ni tofauti sana na baadhi ya makabila ya Kiafrika ambayo miaka ya nyuma yaliona kuzaa mapacha k**a uchuro ambapo wengine waliuawa.
Utunzaji wa mtoto Utunzaji na malezi ya watoto kwa Wanyaturu ulitofautiana kulingana na jinsi ya mtoto. Apozaliwa mtoto wa kiume, watu walikata miti na kumletea nyumbani, hii ni kuonyesha kuwa atakuwa mjengaji wa nyumba na atakuwa na z**i la ng’ombe.
Pili mtoto wa kiume aliyezaliwa alikatiwa upinde kuonesha kuwa ni shujaa ambaye atalinda na kupigania nchi yake mpaka kufa.
Tatu wa kiume aliapishwa kuonesha kuwa yeye ni mtawala wa nyumba na familia yake. Kwa upande wa msichana alipozaliwa wanawake wa jamii hiyo walimkatia mzigo wa kuni kwa sababu ndiyo itakayokuwa kazi yake kubwa wakati atakapokuwa mtu mzima na mama mwenye mji. Kwamba jiko ilikuwa ndio ‘ofisi’ ya mtoto wa k**e ili familia iweze kula.

26/06/2017

Tabu Ley maarufu kwa jina na Rochereau, alizaliwa mwaka 1940 huko Bandundu katika Jamhuri ya Demokrasi ya Kongo. Alianza maisha akiitwa Pascal Emmanuel Sinamoyi Tabu, jina la Rocherau lilikuwa ni jina la utani toka shuleni na ndilo alilolitumia alipopeleka nyimbo zake za kwanza kwa Joseph Kabasele wakati akiomba kujiunga na bendi ya African Jazz. . Tabu Ley alianza maisha yake ya muziki mapema sana na 1954 akiwa na umri wa miaka 14 tu aliandika wimbo wake wa kwanza Bessama Muchacha, ambao akaurekodi na kundi maarufu la African Jazz lililokuwa chini ya Joseph ‘Grande Kalle’ Kasebele, (asichanganywe na Pepe Kalle). Aliendelea na shule na hatimae alipomaliza High School 1959, ndipo alipojiunga rasmi na African Jazz. Alikuwa mmoj awapo wa walioimba ule wimbo utunzi wa Grande Kalle, na uliotikisa anga la Afrika miaka ya 60, Independence Cha Cha. Uliogeuka na kuwa wimbo rasmi wa kusherehekea uhuru wa kongo Baada ya kiasi k**a miaka minne alijiengua bendi hii na akiwa na mpiga gitaa mahiri Nicholaus Kassanda aka Dr Nico, wakaanzisha African Fiesta, ambapo alikuweko hadi 1965, wakati Kongo imewaka moto kimuziki na ushindani kuwa mkali sana, akaachana na Dr Nico na kuanzisha African Fiesta National au mara nyingine ikiitwa Africa Fiesta Flash, Wanamuziki k**a Papa Wemba na Sam Mangwana ni kati ya wakongwe waliowahi kupitia katika kundi hili tishio.
Kufikia mwaka wa 70, Tabu Ley alianzisha Orchestre Afrisa International wakati huo Afrisa na TPOK Jazz ndizo zilikuwa bendi maarufu zaidi Afrika. Afrisa waliteremsha vibao k**a Sorozo, Kaful Mayay, Aon Aon, na Mose Konzo na Tabu Ley aliweza hata kupata tuzo toka serikali za nchi k**a Chad iliyompa heshima ya Officer of The National Order, wakati Senegal ilimpa heshima ya Knight of Senegal, na akawa sasa anaitwa Siegneur Rochereau. Katikati ya miaka ya 80 Tabu Ley aligundua kipaji cha mwanamama aliyekuja kutikisa anga za Afrika naye si mwingine ila Mbilia Bel, baadae Tabu alimuoa Mbilia a wakapata mtoto mmoja. Nyimbo k**a Nadina, Nakei Nairobi zinaonyesha kipaji gani alikuwa nacho binti huyu aliyekuwa mzuri kwa sura, aliyejua pia kucheza na kutawala jukwaa vizuri. 1988 Tabu akamgundua muimbaji wa k**e mwingine Faya Tess. Hapo Mbilia akaacha bendi na kuendelea na maisha yake ya muziki peke yake.
Kipindi hiki, mtindo wa Soukus uliokuwa na mapigo yenye mwendokasi zaidi ya lile rumba la Afrisa na TPOK Jazz ulianza kuzishika nyoyo za vijana, bendi hizi kubwa zikaanza kufifia.

Mwanzoni mwa miaka ya 90 Tabu Ley alihamia Marekani akaishi Kusini mwa California, akabadili muziki wake katika kujaribu kujikita zaidi katika soko la ‘Kimataifa’, akatunga nyimbo k**a Muzina, Exil Ley, Babeti Soukous. 1996 Tabu Ley alishiriki katika album ya kundi la Africando na kushiriki katika wimbo Paquita wimbo aliyokuwa ameurekodi miaka ya 60 akiwa na African Fiesta. Tabu alipata cheo cha Uwaziri katika utawala wa Laurent Kabila baada ya kuondolewa kwa Mobutu. Hata baada ya kifo cha Laurent Kabila November 2005 Tabu alipewa cheo cha Vice-Governor in charge of political, administrative, and socio-cultural questions, kwenye jiji la Kinshasa.

Mwaka 2006 Tabu Ley akashirikiana na rafiki yake wa muda mrefu Maika munah na kutoa album yake ya mwisho iliyoitwa Tempelo, katika album hiyo kuna wimbo ambao ni k**a kumbukumbu ya kote alikopita na pia akaimba wimbo mmoja na binti yake Melodie.

Mwaka 2008 alipata mshtuko wa moya na hakika kuanzia hapo hali yake haikutengenemaa mpaka kifo kilipomchukua siku ya Jumamosi Nov 30 2013, katika hospital ya St Luc Bsusells Ubelgiji. Matatizo ya kisukari na moyo yalisababisha kifo cha mbuyu huu wa muziki wa rumba. Inasemekana tabu Ley alikuwa na watoto wengi sana, inasemekana walifikia 104. Hata mwenyewe alipokuwa hai akiulizwa ana watoto wangapi hakujua. Watoto wake wachache walifuata nyayo za baba yao, akiwemo Melodie, binti aliyezaa na Mbilia Bel ambae sauti yake imo katika album ya mwisho ya Tabu Ley ‘Tempelo’ aliyoitoa mwaka 2006. Wengine katika muziki ni

Pegguy Tabu, Abel Tabu, Philemon and Youssoupha Mabiki.

Youssoupha ni rapper anaeishi Paris, alizaliwa mwaka 1979 , mama yake alikuwa kutoka Senegal. Mwanae Marc Tabu ni mtangazaji kwenye TV moja huko Paris na ndie aliyetoa taarifa ya kwanza ya kifo cha baba yake kwenye ukurasa wake wa Facebook mwaka 2013.

25/06/2017

Ukiniambia nikutajie majina matano ya wanamuziki ambao nawaita “vinara” nchini Tanzania,bila shaka kabisa jina la Muhidin Maalim Mohamed Gurumo halitokosa.Gurumo ni hazina.Ni mwanamuziki ambaye alikua ana sifa ya pekee ya kudumu katika bendi moja bila kuhama kwa muda mrefu kupita kawaida. Hii ni tofauti kabisa na wanamuziki wengi ambao kila kukicha hubadilisha bendi.

Mwanamuziki huyo alizaliwa Masaki Kisarawe mwaka 1940 na kupata elimu yake ya msingi katika shule ya msingi Sungwi huko huko Kisarawe, na baadae aliacha shule baada ya baba yeke kufariki na kukosa mtu wa kumgharamia mahitaji ya shule.

Baada ya kuacha shule kutokana na kufiwa na baba yake, Gurumo mwaka huo huo alijiunga na bendi ya mtaani iliyojulikna k**a Scock Jazz iliyokuwa na maskani yake katika mitaa ya Moshi na Kigoma
Mwaka mmoja baadae alijiunga na bendi ambayo ilikuwa na vyombo vya kisasa wakati huo, iliyojulikana kana k**a Kilimanjaro Chacha, ambako alitunga vibao k**a vile Twende Tukalime, Mapenzi Hayana Dawa, Ushirikina ni Sumu na Maendeleo.

Mwaka 1963 Gurumo alijiunga na Rufiji Jazz Band, ambako alitunga kibao cha Uwezo wa Binadamu Kufikiri, ambacho kilimpatia umaarufu mkubwa kufuatia kupenda na wapenzi wengi wa muziki wa dansi.

Baadae mwaka huo huo alijiunga na bendi ya Kilwa Jazz na kutunga kibao cha Wewe Mpenzi Naomba Unishauri Kabla Hatujagombana, na kile cha siwezi Kukununulia gari wakati hata baiskeli Sina
Mwaka 1964 alikuwa miongoni mwa waanzilishi wa bendi ya Nuta Jazz, baadhi yao ni akina Ahmed Omary, Mohamed Omary, Epimakus Mkundika na Rashid Abdallah (wengine wako hai na wengine wameshafariki).

Akiwa na bendi hiyo ya Nuta Jazz, Gurumo alitunga vibao vingi lakini baadhi yake ambavyo alivikumbuka ni Magdalena, Maneno ya Mwalimu Maneno ya Wazee Yote Sawa, Rehema Umefeli Shule kwa Kisa Gani? na vibao vingine.

Baadae bendi hiyo ilibadilishwa jina na kuitwa Jumuiya ya Wafanyakazi, JUWATA, ambapo akiwa na bendi hiyo baadhi ya vibao alivyotunga ni Dada Fatuma, Dada Sabina na vingine vingi kabla haijabadilishwa na kuwa Ottu Jazz Band.

Address

Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Africa moto posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share