03/01/2023
Kwanini Taa ya Check engine huwaka?
Kwenye gari zipo sababu nyingi zinaweza kuwasha taa ya Check engine, mfano;
1.Kufa kwa sensors na components zingine za umeme/electronics
2. Kukatika kwa wires.
3. Kuvuja kwa hewa (Vacuum leak).
4. Kubadilika kwa taarifa za vifaa ambavyo vipo calibrated.
5. Baadhi ya vitu kufanya kazi chini ya kiwango.
6. Poor electrical contact kwenye connectors ambayo mara nyingi husababishwa na uchafu, kutu n.k.
7. Na mengine mengi sana.
Hivyo hata suala la urekebishaji wa matatizo ya check engine, hutofautiana kulingana na aina ya tatizo na zipo namna nyingi za kurekebisha k**a kubadili kifaa, kuunga wires, kusafisha, calibration, n.k.
Gari inaweza kuwasha taa hiyo na mtu akaona au asione mabadiliko yoyote kwenye gari, mfano taa hiyo inaweza ikawaka na ikaja na mabadiliko yafuatayo.
1. Engine kukosa nguvu
2. Engine kumisi(misfire)
3. Kelele kwenye engine
4. Kujizima
5. Kutetemeka
6. Kutoa moshi mwingi
7. Kusumbua kuwaka
8. Kutumia mafuta mengi
9. Rough Idle (Gari haitulii sailensa)
10. Kushtuka wakati unaendesha.
Zipo nyingi sana.
Kwa kifupi kitu chochote kikiharibika kwenye engine hii taa inaweza kuwaka hivyo inakuwa ni ngumu kukisia hiyo taa imewaka kwanini, ni mpaka pale tutakapofanya diagnosis.
Pia Unaweza kupata matatizo niliyokueleza hapo juu lakini gari isiwashe taa yoyote kwenye dashboard. Hivyo siyo kila tatizo litawasha taa ya Check engine. Lakini ukifanya diagnosis inaweza kuonekana muda mwingine.
Check engine huwaka endapo kuna tatizo kwenye engine. Gari nyingi za Toyota na gari zote zinazotumia ECU moja kwa engine na gearbox, check engine huwaka kwa sababu ya tatizo kwenye engine au gearbox.
Karibu kwetu kwa huduma hizi...
1. Kufanya diagnosis na marekebisho ya matatizo yote yanayowasha taa za tahadhari kwenye dashboard mfano check engine, n.k.
Engine Diagnosis ni Tsh. 30,000/=
Full Systems ni Tsh. 50,000/=.
2. Kufunga GPS trackers na vifaa vya kuzuia wizi wa vyombo vya moto k**a Kill switch na Immobilizer kwa bei nafuu.
Gari ndogo aina yoyote na kampuni yoyote.
Tupo Dar es salaam, Magomeni, Mwembechai.
Simu/Whatsapp: 0621 221 606 au 0688 758 625.